Radio Salaam ilianza kupeperusha mawasiliano yake kutoka jijini Mombasa, 12:00pm tarehe 16-11-2006, saa; kipindi cha kwanza kwenda hewani kikiwa Mpasho wa Radio Salaam.
Radio Salaam imekubalika na kwa habari za kuaminika za kimkoa, kitaifa na kimataifa.
Kauli Yako, Farashani, Uteo, Dini ya Mitume, MV Salaam na Jukwaa Wazi,na Kongamano ni baadhi ya vipindi vyetu vilivyopata umaarufu si haba, miongoni mwa wasikilizaji na wadhamini wetu.
Vipindi hivi vinalenga kuboresha jamii kupitia mada mbalimbali, hasa kuhusiana na siasa, uchumi, matukio ulimwenguni, michezo, masaala tata ya kijamii, miongoni mwa masaala mengine mengi.
Uwezo wa Radio Salaam, kibiashara
Tuna uhusiano wa kudumu wa moja kwa moja na wasikilizaji wetu ambao ni 300,000 na zaidi,kutoka matabaka mbali mbali ya kijamii, kiuchumi na kidini wanaotegea stesheni hii, kila wiki.
Vifaa vya kisasa: Tunaweza kupeperusha matangazo kutoka mahali popote pale nchini kupitia gari letu la OB Van lenye mitambo ya kisasa.Redio Salaam ndio stesheni pekee yenye gari la aina hii kati ya vituo vyote hapa Pwani.
Matokeo: Tumetambulika kwa halfa mbalimbali zinazotujumuisha moja kwa moja na wasikilizaji wetu hapa Pwani. Hafla hizi ni nafasi mwafaka ya kuwafkia wateja wako kwa huduma na bidhaa zako.
Tutuma ujumbe kupitia dawati letu la biashara kupitia barua pepe kwa: sales@radiosalaamfm.com
Pamoja, tunaweza kuunda mpango murwa wa kibiashara, wenya kukunufaish kimauzo. Fanikisha mauzo katika biashara yako kwa ulimwengu, kupitia Radio Salaam!