Current Affairs

Dereva wa mojawapo ya magari yaliyotumiwa na wavamizi wa mpeketoni alifikishwa katika mahakama kuu mjini Mombasa na kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya Zaidi ya watu 12. Hatahivyo, Dyana Salim alikanusha mashtaka hayo. Dyana anadai kuwa alitekwa nyara na wavamizi hao na kupokonywa gari lake kabla ya wao kutekeleza mauaji hayo. Kesi yake itasikilizwa tena siku ya Jumatatu.
Inspekta Jenerali wa polisi David Kimayo awaamuru makamishna wa kaunti zote kuboresha usalama wakati wa mkutano wa kisiasa uliyopangwa na upinzani maarufu kama saba saba.
Mawaziri wa afya kutoka nchi tofauti za Afrika wakutana jijini Accra huko Ghana kwa kikao cha dharura kinachotazamiwa kujadili mkurupuko wa maradhi ya ebola nchini Guinea, Liberia na Sierra Leone. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kufikia sasa kumeripotiwa visa 759 vya maambukizi.
There are no comments