A PHP Error was encountered

Severity: Notice

Message: Only variable references should be returned by reference

Filename: core/Common.php

Line Number: 272

Je Wajua? MAELEZO YA KWELI | Blog
Fun!

Insights

MAELEZO YA KWELI YANAYOTISHA!


Pindi unapoamka ghafla usingizini usiku wa manane, juwa kuna uwezekano wa 85% kuwa kiumbe fulani chumbani kinakuangalia wakati umelala. Kwa hivyo hakikisha umeswali swala ya Ishaa na kusoma kabla hujalala.

Kwa rehema yake Mungu, kuna kifuniko machoni mwa kila binadamu kinachomzuwiya kuona malaika na majini peupe. Kifuniko hicho Mungu hukiondoa tu pindi mtu anapokufa. Hapo utakuwa kwenye 'hayatul barzakhiyyah' na kuweza kuwaona!

Pindi mtu anapojiburudisha kwa kusikiza nyimbo zenye zana za muziki, basi hapo huhudhuria majini na mashetani wakazunguka kinachotoa sauti na kuanza kucheza au kudansi! Lau ungelifunguliwa hicho kifuniko na kuwaona, ungeogopa na kupasukwa na roho na labda kuzirai au kufa kabisa. Kwa hivyo fikiriana mara mbili kabla ya kusikiza muziki.

Kila alfajiri ya siku tukufu ya Ijumaa, wanyama wote duniani huwa kimya wakingojea kusikia parapanda ya siku ya qiyama! Mungu atupe husnul khaatimah.

Katika mwaka wa 1997 kulitokea sauti ya kutisha sana na kubwa kutokea upande wa bahari ya Pacific. Sauti hiyo ilisikika masafa 5000km kutoka baharini, na mpaka sasa hakuna anayejua chanzo cha sauti hiyo.

Usitembee kwa miguu iliyokufa ganzi wala kuegemea mkono ambao umekufa ganzi, huenda mifupa ikavunjika na ilhali hujui.

Kuna uwezekano binadamu akapoteza nuru ya macho na kuwa kipofu pindi atakapokaa kwa giza kali kwa muda ya siku tatu mfululizo.

Pindi unapo ota kuwa unaanguka kisha mwili wako ukatingishika na kushtuka, basi juwa akili imefanya kazi yake ya kukuzindua, la sivyo viungo vyote vya mwili vilikuwa vyasimama na kufa kabisa. Umenusurika!.

Wakati anapokufa mwanadamu huwa kuna zoezi fulani katika ubongo wake kwenye upande wa kushoto linaendelea kwa muda wa dakika 7. Zoezi hili huwa linamkumbusha aliyekufa kwa haraka sana yote aliyoyatenda duniani alipokuwa bado yuko hai, kisha linazima!

Kuna harakati nyingi ndani ya mwili wa binadamu aliye hai zinazosababishwa na viungo vya ndani. Ikiwa wataka kusikiza harakati hizo, ziba masikio yako yote mawili. Kisha sikiza.

Kinga yako ya mwili inauwa (kuharibu au kubomoa) 'cell' moja kwa uchache kila siku. Kwa ajili 'cell' hiyo ingewachwa basi ingekuwa ni sababu ya mtu kupata ugonjwa wa sararani (cancer)!

Hebu daima tusemeni 'SubhanaAllah walhamduLillah'.
 

photo credit: -Reji via photopin cc

Comments

There are no comments

Post a comment