Insights
TAHADHARI – Picha za taarifa hii huenda zikakukirihisha.
“Jina langu ni Hassan Ali. Nina miaka 70. Maisha yangu yote nimekuwa mraibu wa tambu na mao. Sasa najuta sana kutumia uraibu huo. Hivi sasa niko kitandani hospitali ya Pandya mjini Mombasa nikiwa mgonjwa wa saratani ya mdomo (mouth cancer) iliyosababishwa na uraibu huo. Siwezi kula, siwezi kunywa, siwezi kucheka, siwezi kusema. Chakula kikubwa nipewacho ni maji tena nanyishwa vitone vitone kwa sindano kama mtoto wa ndege. Madaktari wameshindwa kunitibu. Nimekwenda mpaka India nikaambiwa nirudi kwetu Mombasa na nisubiri siku yangu ya kukutana na Maulana. Sina dawa ila ni kungoja siku yangu ifike. Leo mjukuu wangu Ahmed Juma Bhalo alikuja na wenzake kunitembelea na kunichangia damu. Nawashukuru sana. Sasa basi mimi kama babu yenu nachukuwa fursa hii kuwaomba muwachane na uraibu wa aina yoyote. WALLAHY hakuna uraibu mzuri. Nimempa Ahmed ruhusa ya kunipiga picha na kuwaonesha nyinyi wajukuu zangu ndio mushuhudie nisemacho. Na mukitaka njooni munione hospitalini. Mwenyewe niko radhi na nitafurahi mukija kunitembelea. Naomba dua zenu kwa wingi. Shukran sana.” END.
photo credit: Curtis Gregory Perry via photopin cc
“Jina langu ni Hassan Ali. Nina miaka 70. Maisha yangu yote nimekuwa mraibu wa tambu na mao. Sasa najuta sana kutumia uraibu huo. Hivi sasa niko kitandani hospitali ya Pandya mjini Mombasa nikiwa mgonjwa wa saratani ya mdomo (mouth cancer) iliyosababishwa na uraibu huo. Siwezi kula, siwezi kunywa, siwezi kucheka, siwezi kusema. Chakula kikubwa nipewacho ni maji tena nanyishwa vitone vitone kwa sindano kama mtoto wa ndege. Madaktari wameshindwa kunitibu. Nimekwenda mpaka India nikaambiwa nirudi kwetu Mombasa na nisubiri siku yangu ya kukutana na Maulana. Sina dawa ila ni kungoja siku yangu ifike. Leo mjukuu wangu Ahmed Juma Bhalo alikuja na wenzake kunitembelea na kunichangia damu. Nawashukuru sana. Sasa basi mimi kama babu yenu nachukuwa fursa hii kuwaomba muwachane na uraibu wa aina yoyote. WALLAHY hakuna uraibu mzuri. Nimempa Ahmed ruhusa ya kunipiga picha na kuwaonesha nyinyi wajukuu zangu ndio mushuhudie nisemacho. Na mukitaka njooni munione hospitalini. Mwenyewe niko radhi na nitafurahi mukija kunitembelea. Naomba dua zenu kwa wingi. Shukran sana.” END.

photo credit: Curtis Gregory Perry via photopin cc
There are no comments